Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali kuboresha mfumo wa utoaji tiketi U-DART

Ijumaa , 27th Mei , 2016

Serikali imesema kuwa itaufanyia marekebisho ya haraka mfumo wa utoaji risiti na changamoto nyingine katika mradi wa mabasi yaendayo haraka(U-DART),ili mradi huo utoe tija ya haraka kama inavyohitajika.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa ndani ya basi la Mradi wa Mabasi yaendayo haraka UDART.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika mradi huo Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amesema kuwa zipo changamoto ambazo ameziona mara baada ya ziara hiyo ambazo serikali itazifanyia kazi ili kuboresha zaidi usafiri huo.

Aidha Waziri Mkuu Majaliwa amewataka watumishi wa mradi huo kufuata sheria ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua wananchi ambao wameonekana sio waaminifu kwa kufanya udanganyifu wa kurejea vituo na tiketi za siku iliyopita.

Waziri Mkuu Majaliwa amesema baada ya mradi huo kuboreshwa zaidi itakua haina ulazima wa watu kwenda na magari yao mpaka mjini hivyo watatakiwa kupaki nje ya mji na kutumia usafiri huo kuelekeza kwenye shughuli zao za kila siku.

Kwa upande wake Kamanda wa Kikosi cha Usalama barabarani, Mohammed Mpinga, amewataka watumiaji wa barabara kufuata sheria na kuacha kuzitumia njia hizo na endapo mtu akikiuka adhabau kali itachukuliwa dhidi yake.

Aidha, Kamanda Mpinga ameongeza kuwa jeshi la Polisi na Kikosi cha usalama barabarani wataendelea kutoa elimu kwa Wananchi watembea kwa miguu ili waelewe matumizo ya barabara hizo ikiemo kutumia vivuko pindi wakitaka kuvuka barabara.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea