Jumatatu , 21st Nov , 2022

Serikali kupitia wizara ya Tamisemi imeagiza halmashauri zote nchini kukamilisha agizo la baraza la makatibu wakuu la kuunda sheria ndogondogo zitakazo saidia kupambana na ukatili wa kijinsia anbao umetajwa kuongezeka siku hadi siku hapa nchini 

Maagizo hayo yemetolewa leo na mratibu wa masuala ya jinsia kutoka Tamisemi Linus Kahandaguza pa moja na mkuu wa wilaya ya  Ubungo Kheri James wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha wataalam wa bajeti katika halmashauri kilichoandaliwa na mtandao wa jinsia nchini  ambapo wamesema kwa sasa kumekuwa na ongezeko la vitendo vya ukatili nchini hivyo ni vyema kukachukuliwa hatua za haraka ikiwemo uundaji wa shwria hizo ndogondogo pa moja na uwekaji mipango katika bajeti za halmashauri zitakazo zingatia masuala ya usawa wa kijinsia .

Kwa upande wake mkurugenzi wa mtandao wa jinsia nchini lilian liundi pamoja na mwenyekiti wa halmashauri ya Same Yusto Mapande wamesema katika kikao hicho wamekutanisha madiwni na maafisa maendeleo na mipango kutoka halmashauri 14  ambapo watapata mafunzo juu ya namna ya kutenga bajeti zenye kulenga usawa wa kijinsia ambapo kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2016 zaidi ya dola za kimarekani bilioni 105 zimekuwa zikipotea kutokana na kutokuwepo bajeti  za usawa wa kijisnia .

Nao baadhi ya madiwani kutoka halmashauri za Mbeya na Kishapu ambao wametajwa kuwa moja ya halmashauri zilizofanikiwa kutengeneza bajeti za usawa wa kijinsia wamesema halmashauri hizo  zimefanikiwa kutenga fedha kwa ajili kutatua masuala ya usawa wa kijisnia ikiwemo kuja na shule maalumu za wasichana ..