
Imeelezwa kuwa mshtakiwa huyo amesahaulika gerezani
Zumaridi na wafuasi wake wanakabiliwa na kesi ya kuwazuia maafisa wa serikali kutekeleza majukumu yao na kuwajeruhi Askari Polisi
Wakili wa utetezi Linus Amri ameiomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kusikiliza shauri hilo kwani wasingeweza kujitetea bila idadi ya washtakiwa kutimia
Aidha katika shauri namba 11 linalomkabili Zumaridi dhidi ya Jamhuri, wakili wa upande wa Jamhuri Martha Mwadenya ameomba kupangwa tarehe nyingine kwani upelelezi bado haujakamilika katika shauri hilo.
Baada ya wakili huyo kudai upelelezi bado haujakamilia Hakimu mkazi mwandamizi Boniventure Lema ameiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 14 Novemba mwaka huu itakapotajwa tena