Jumatano , 2nd Mar , 2022

Jeshi la Polisi mkoa wa Kagera, linamshikilia mwanaume aitwaye Anderson Clemence (35), mkazi wa kijiji cha Kafunjo, Kata ya Kamagambo wilayani Karagwe kwa tuhuma za kumuua mtoto wake Hansen Anderson, mwenye umri wa miezi minne kwa shoka.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera, Wankyo Nyigesa

Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Wankyo Nyigesa, amesema kuwa baba huyo alikamatwa Machi 01, 2022 na kwamba chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi baina yake na mke wake, uliosababisha arushe shoka hilo kumpiga mke wake na badala yake likampiga mtoto huyo aliyekuwa amebebwa mgongoni na mama yake mzazi.