Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sugu amtaja Mbowe, CCM kwenye hotuba yake

Jumatatu , 22nd Apr , 2019

Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi almaarufu kama Sugu alipendekeza kurejeshwa kwa baadhi ya viwanja vya michezo vinavyomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi kwa kile alichokidai kuwa viwanja hivyo vilimilikiwa wakati wa mfumo wa chama kimoja.

Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi

www.eatv.tv imekuletea baadhi ya vipengele ambavyo kambi hiyo ya upinzani ilivipendekeza kupiria bajeti yake kivuli ya Wizara hiyo ambapo Mbunge Sugu alishindwa kuisoma kutokana kuondolewa na baadhi ya maneno.

"Mheshimiwa Spika, kanuni za kudumu za Bunge, napenda kuwasilisha maoni ya Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni  (KUB) kuhusu bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kutoa pole na hongera Freeman Mbowe kwa kukaa gerezani kwa miezi 3, ameonyesha ukomavu na umahiri katika uongozi kwani kwa muda wote huo, aliendelea kukiimarisha chama, na kukifanya kuwa na mshikamano." ilisema sehemu ya bajeti hiyo ya Sugu

Sugu alieleza kuwa "siwezi kuwasahau wapiga kura wa  Mbeya, kwa jinsi wanavyonipa ushirikiano kwa hali zote, ninawashukuru zaidi hasa kwa kufunga mjadala kuhusu ubunge Mbeya Mjini, hii nawaibia siri wale wanaotaka kugombea ubunge Mbeya Mjini suala hilo lilishaamuliwa na kufungwa na wananchi wa Mbeya kwa hiyo wakajaribu kwengine"

Kuhusiana michezo

"Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka CCM kuacha mara moja kuingiza itikadi za kisiasa za chama chao  katika michezo kwani kwa kufanya hivyo inaweza kufifisha morari kwa baadhi ya wachezaji ambao si wanachama wa CCM, wala mafanikio yao hayatokani na chama wala Serikali ya CCM, bali ni juhudi zao binafsi" ameandika Sugu

Mapendekezo

Sugu amesema kuwa "viwanja vyote vya michezo vilivyopatikana na kumilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kabla ya mwaka 1992, (siasa ya vyama vingi ilipoanza), virejeshwe Serikalini, ili viweze kuendelezwa kwa ajili ya kukuza sekta ya michezo nchini."

Alhamis ya wiki iliyopita Bungeni Jijini Dodoma Mbunge huyo wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi aligomea kuendelea kusoma hotuba hiyo kwa kile alichokidai kuondolewa kwa baadhi maneno ambayo aliyaandika

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa