Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tanzania na Kenya wafafanua suala la kuzuia Ndege

Jumamosi , 1st Aug , 2020

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini (TCAA), Hamza Johari, amesema kuwa sababu iliyopelekea na wao kuzizuia Ndege za Kenya kutua nchini ni baada ya nchi hiyo kuzuia ndege za Tanzania kutua kwao na kuongeza kuwa hali ya namna hiyo ni kawaida katika biashara.

Waziri wa Uchukuzi wa Kenya, James Macharia na kulia ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Anga nchini, Hamza Johari.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Agosti 1, 2020, wakati akizungumza kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya Eats Africa Radio na kuongeza kuwa, nchi ya Kenya ilikuwa imeomba ruhusa ya Ndege zake kutua nchini kuanzia leo, lakini wao walishangazwa kuona Kenya yenyewe imezuia ndege za Tanzania hivyo na wao wakaamua kuchukua maamuzi ya sawa kwa sawa.

"Tumefikia uamuzi huo kwa sababu katika sheria na taratibu zinazosimamia uendeshaji wa usafiri wa anga kati ya nchi na nchi ni kwamba, Mataifa yanatakiwa yawe sawa kwa sawa, Kenya walikuwa wameomba kuja Tanzania kuanzia leo kutua katika viwanja vya Dar es Salaam, Zanzibar na Kilimanjaro na sisi hatukuwa na tatizo tukawapa ruhusa, lakini baadaye tukasikia wao wanatuzuia sisi tusiende kule" amesema Johari.

Aidha Mhandisi Hamza ameongeza kuwa "Mwaka 2015 walizuia gari za watalii zisiingie Kenya, kwahiyo tukafanya hivyo na baada ya siku mbili wao wakaondoa kikwazo walichotuwekea, tumetendewa kitu ambacho si sahihi na sisi inabidi tufanye hivi badala ya kukaa kimya na kuwaacha wao waendelee kufanya wanachotaka".

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, amesema kuwa siku ya Jumanne kutakuwa na mkutano na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ili wajue nini chanzo kilichopelekea nchi ya Kenya kuzuia Ndege za Tanzania zisitue nchini humo.

Aidha East Africa Radio ilimtafuta Waziri wa Uchukuzi wa Kenya, James Macharia, ambaye alikataa katakata kama nchi yao imezuia Ndege za Tanzania kutua nchini humo.

"Hakuna ndege ya Tanzania ambayo imezuiliwa kuingia Kenya, sisi tulisema hizo nchi tulizoziweka kwenye hiyo orodha watu wao wakifika hapa hawatakaa karantini, lakini kama nchi haipo kwenye hiyo orodha watawekwa Karantini, sisi taarifa ya kuzuiwa kuingia Tanzania tumeipata lakini tutazungumza na wenzetu na tutasikilizana" amesema Waziri wa Kenya.

 

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya