Soko la hisa
Taarifa hiyo imetolewa leo Oktoba 7, 2019 na Meneja Miradi wa Soko la Hisa la Dar es Salaam(DSE) Emmanuel Nyalali, ambapo amesema kuwa hisa za Vodacom ndiyo chanzo cha kuongezeka kwa thamani hiyo baada ya wawekezaji wawili wakubwa kuuziana hisa.
''Mpaka sasa kwa mwaka 2019, ni kaunta ya vodacom ndiyo imechangia 85.11 ya thamani ya mauzo ya hisa, ikifuatiwa na TBL kwa asilimia 12.52 na CRDB kwa asilimia 1.69, ambapo kaunta ya Vodacom imechangia kwa asilimia 85.50 ya idadi ya hisa zilizouzwa sokoni, ikifuatiwa na kaunta ya CRDB kwa asilimia 12.93 na TBL asilimia 1.02'', amesema Nyalali.
Kwa sasa thamani ya hatifungani zilizoorodhesha kwenye Soko la Hisa, zilifikia Shilingi trilioni 10.40, ambayo ni sawa na hatifungani za Serikali zenye thamani ya Shilingi trilioni 10.22 na hatifungani zilizotolewa na makampuni sawa na thamani ya Shilingi bilioni 176.