Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ukarabati kituo cha umeme Kipawa karibu kukamilika

Jumapili , 31st Aug , 2014

Kazi ya ukarabati wa kituo kikubwa cha kusambazia umeme cha Kipawa ambacho kilipata hitilafu na kuharibika juzi saa Saba usiku inaelekea kukamilika baada ya maeneo mengi yaliyoathiriwa na hitilafu hiyo kuanza kupata umeme.

Meneja wa Tanesco Mkoa wa Ilala, Mhandisi Atanasius Nangali.

Meneja wa Tanesco mkoa wa Ilala mhandisi Atanasius Nangali, ameiambia East Africa Radio kuwa kazi ya ukarabati inaendelea vizuri ambapo mafundi wa shirika hilo wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana kuhakikisha umeme unarejea.

Ameyataja maeneo ambayo bado umeme haujarejea mpaka sasa kuwa ni Gongolamboto, Kivule na Kipunguni na kwamba muda wowote kuanzia sasa umeme katika maeneo hayo utarudi katika hali yake ya kawaida.

Kwa mujibu wa mhandisi Nangali, hitilafu hiyo ilisababisha maeneo mengi ya wilaya za Temeke, Ilala na Kisarawe kukosa nishati ya umeme, na kwamba juhudi zilifanyika za kurejesha umeme katika maeneo nyeti ikiwa ni pamoja na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere ambako mafundi wa TANESCO mkoa wa Ilala waliandaa njia ya moja kwa moja ya umeme kutoka maeneo mengine ya jiji kuelekea uwanjani hapo.

Aidha, mhandisi Nangali amesema hitilafu hiyo ni ya kiufundi na kuongeza kuwa matukio ya aina hiyo yamekuwa nadra hivi sasa kwani shirika limeimarisha ukarabati wa miundombinu yake ikiwa ni pamoja na njia zilizochakaa pamoja na mifumo ya usambazaji.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita