Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ukiukwaji haki za binadamu bado tatizo Tanzania

Alhamisi , 31st Jul , 2014

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimesema kumekuwa na ongezeko kubwa la ukiukwaji wa haki za binadamu nchini ambapo kwa mwaka huu watu wapatao 320 wameuwawa ikilinganishwa na watu 303 mwaka jana.

Mkurugenzi mkuu wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu - LHRC Dkt Hellen Kijo- Bisimba.

Mtafiti wa LHRC Bw. Pasiance Mlowe amesema hayo leo jijini Dar es Salaam na kufafanua kuwa wengi kati ya watu hao wameuawa kutokana na imani za kishirikina.

Kwa mujibu wa Mlowe, ongezeko kubwa la watu kujichukulia sheria mikononi, mauaji ya imani za kishirikina na mauaji ya watu wenye ulemavu yanatokana na kukosekana kwa elimu ya haki za binadamu katika mfumo wa elimu nchini.

Kwa upande wao wananchi waishio maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam wakiongea na East Africa Radio wamesema kutokutenda haki kwa wasimamiaji wa sheria ikiwemo mahakama na polisi kumeongeza hali ya wananchi kujichukulia sheria mkononi ambapo wameitaka serikali kutoa elimu kuhusu haki za binadamu wanaojichukulia sheria mkononi kudhibitiwa.

Wakati huo huo, watuhumiwa 25 wa matukio ya ulipuaji wa mabomu katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Olasit, mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Bar ya Arusha Night Park , Mgahawa wa Vama na umwangiaji wa tindikali kwa baadhi ya watu, wanatarajia kufikishwa Mahakamani hapo kesho.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, jijini Arusha Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Liberatus Sabas amesema katika tukio la ulipuaji bomu Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Olasiti lilitokea Mei 5 mwaka 2013 ambapo watu zaidi ya 16 walijeruhiwa na watatu kufariki dunia,

Kamanda Sabas amesema tukio la kurushwa bomu nyumbani kwa Sheikh Sudi Aly Sudi lilitokea Julai 3 mwaka huu na watuhumiwa wengine kumi watafikishwa mahakamani kwa tukio la kupatikana na mabomu saba nyumbani Julai 21 mwaka huu, huku watuhumiwa watatu, watafikishwa mahakamani kwa kuhamasisha vitendo vya kigaidi kupitia mtandao wa kijamii

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa