Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wadhamini wa Lissu waonywa, Mahakama yagoma

Jumatatu , 25th Feb , 2019

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, ametoa onyo kwa wadhamini wa mtuhumiwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kufika mahakamani kila kesi inapotajwa, baada ya kukataa ombi la Wakili wa upande wa Jamhuri la kutoa hati ya kumkamata kiongozi huyo.

Kutoka kushoto, Jabir Idrissa, Mhariri wa Mawio, Simon Mkina, Mhariri na Mmiliki wa gazeti la Mawio na Tundu Lissu walipokuwa mahakamani.

 Upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili Simon Wankyo, alidai kuwa Lissu yuko nje ya nchi siyo kwa matibabu, bali kwa ajili ya kufanya kazi za kisiasa na kufikia hatua ya kuiomba mahakama hiyo itoe hati ya kumkamata Lissu.

"Kama itakupendeza mheshimiwa hakimu tunaiomba mahakama yako itoe hati ya kumkamata mshtakiwa kwa kuwa tunamuona anazunguka nchi mbalimbali kufanya mihadhara," amedai Simon.

Baada ya Wankyo kueleza hayo, Hakimu Simba amesema hati ya kumkamata mshtakiwa kwa sasa haiwezi kutolewa na mahakama hiyo.

"Hati ya kumkamata mshtakiwa kwa sasa haiwezi kutolewa, hivyo nawaonya wadhamini kufika mahakamani kila kesi hii inapotajwa", amesema Hakimu Simba.

Lissu kwa sasa yuko nje ya nchi kwa muda mrefu kwa ajili ya matibabu baada ya kutoka hospitali ya jijini Nairobi, Kenya ambako alikimbizwa baada ya kupata matibabu ya dharura Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana

Lissu na wenzake wanatuhumiwa katika kesi hiyo yenye Na. 208 ya mwaka 2016, kutoa chapisho la uchochezi katika Gazeti la MAWIO, toleo Na. 182 la tarehe 14-20 Januari 2016.

 

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria