Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wafungwa waliosamehewa na JPM wapata shavu

Jumanne , 10th Dec , 2019

Jumla ya wafungwa 79 kati ya wale 5,533, waliosamehewa jana Desemba 9, 2019, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli, wameachiwa huru katika Gereza la Butimba mkoani Mwanza.

Wafungwa walioachiwa huru kwa msamaha wa Rais Magufuli, wakitoka katika Gereza la Butimba, Mwanza.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja tu tangu Rais Magufuli atangaze msamaha huo kwa kile alichokieleza aliguswa sana na maisha wanayoishi wafungwa na kwamba yeye hayupo tayari kuongoza Nchi ya watu wanaolia machozi.

Katika Mkoa wa Mwanza, Rais Magufuli alitoa msamaha kwa wafungwa 190 na leo Desemba 10, 2019, jumla ya wafungwa 79 wameachiwa huru katika Gereza la Butimba na kuagwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, Mkuu wa Gereza la Butimba, Shaku Umba, Kamishina wa Magereza Faustine Kasike pamoja na Mkuu wa Magereza mkoani humo Hamza Hamza.

Mara baada ya kuwaaga wafungwa hao, Mkuu wa Mkoa huo, John Mongella akatoa rai kwao na kuwasihi wakawe raia wema na wasijihusishe na vitendo vya uhalifu.

"Ninawasihi sana mkawe raia wazuri na wema, mkajiepushe na vitendo vya uhalifu ili kuepuka kuvuruga amani ya Mkoa na Nchi kwa ujumla, wengine michango yenu inajulikana mmeshiriki kujenga nyumba nyingi, ninaomba ujuzi mlioupata mkautumie vizuri" amesema RC Mongella.

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera