Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wafungwa waliosamehewa na JPM wapata shavu

Jumanne , 10th Dec , 2019

Jumla ya wafungwa 79 kati ya wale 5,533, waliosamehewa jana Desemba 9, 2019, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli, wameachiwa huru katika Gereza la Butimba mkoani Mwanza.

Wafungwa walioachiwa huru kwa msamaha wa Rais Magufuli, wakitoka katika Gereza la Butimba, Mwanza.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja tu tangu Rais Magufuli atangaze msamaha huo kwa kile alichokieleza aliguswa sana na maisha wanayoishi wafungwa na kwamba yeye hayupo tayari kuongoza Nchi ya watu wanaolia machozi.

Katika Mkoa wa Mwanza, Rais Magufuli alitoa msamaha kwa wafungwa 190 na leo Desemba 10, 2019, jumla ya wafungwa 79 wameachiwa huru katika Gereza la Butimba na kuagwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, Mkuu wa Gereza la Butimba, Shaku Umba, Kamishina wa Magereza Faustine Kasike pamoja na Mkuu wa Magereza mkoani humo Hamza Hamza.

Mara baada ya kuwaaga wafungwa hao, Mkuu wa Mkoa huo, John Mongella akatoa rai kwao na kuwasihi wakawe raia wema na wasijihusishe na vitendo vya uhalifu.

"Ninawasihi sana mkawe raia wazuri na wema, mkajiepushe na vitendo vya uhalifu ili kuepuka kuvuruga amani ya Mkoa na Nchi kwa ujumla, wengine michango yenu inajulikana mmeshiriki kujenga nyumba nyingi, ninaomba ujuzi mlioupata mkautumie vizuri" amesema RC Mongella.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala