Wahamiaji haramu waliokamatwa mkoani Mbeya
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Ulrich Matei amesema watu hao wamekamatwa katika Kijiji cha Namba One kilichopo Kata ya Isongole wilayani Rungwe.
Aidha, Matei amewataka madereva wa magari nchini hasa vijana kuacha kufanya kazi hiyo ya kuwasafirisha wahamiaji haramu hao akidai kuwa ni kosa la jinai kwa mujibu wa sheria na kwamba adhabu yake ni kutaifishwa kwa gari na mhusika kutozwa faini kubwa.