Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Wameambukizwa Ukimwi, nitawasemea" - Matiko

Ijumaa , 15th Mar , 2019

Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko amelituhumu jeshi la polisi kwa kuwafanyia unyanyasaji wa kingono, mabinti na wanawake wanaopelekwa katika vituo vya polisi pindi wanapokamatwa.

Mbunge Esther Matiko

Akizungumza na wanahabari, leo Machi 15, Matiko amesema kwamba, alipokuwa Segerea amekutana na malalamiko ya wanawake ya kwamba wamebakwa na kulawitiwa walipokamatwa na hata kuambukizwa maradhi.

Amesema kwamba vitendo vya unyanyasaji kwa mkoa wa Dar es salaam vimekithiri katika vituo vya Sitaki Shari, Kawe na kile cha Mabatini.

Ameongeza kwamba, "licha ya kulisema suala hili leo mbele ya wanahabari, kama muwakilishi wa wanananchi Bungeni atalifikisha jambo hilo ndani ya bunge ili waathiriwa wa vitendo hivyo wapatiwe haki yao

"Kuna kesi  nyingi sana, mabinti wanabakwa kwenye vituo vya polisi, kulawitiwa na hata kuambukizwa virusi vya ukimwi, nimesema nitalisema hili  bungeni na popote pale mpaka haki za mabinti hawa zitakapopatikana" Amesema Matiko.

Pamoja na hayo Matiko amelalamikia suala la watu wenye magonjwa wa akili kuchanganywa na wemye utimamu katika magereza hasa Segerea na kusema kunaweza kupelekea matatizo kwa mahabusu au wafungwa wengine ndani ya gereza.

Ameongeza kwamba Licha ya matatizo yanayoweza kusababishwa na wagonjwa hao, Serikali inapaswa kutumia sheria ya 'Insanity ACT 31' ambayo inatamka wazi kwamba mtu anayekamatwa akawa na matatizo ya akili apelekwe sehemu stahiki na siyo magereza.

Aidha Matiko amesikitika kuwepo na mahabusu wengi magerezani huku serikali ikitumia gharama kubwa kwa mahabusu ambao hawazalishi huku akisisitiza kwamba wanawake waliopo katika magereza hayo wengine ni wazazi ambao kwa kuwekwa muda mrefu bila kujua hatima ya kesi zao kunapelekea watoto wa mitaani.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi