
Pichani ni zoezi la upimaji macho
Kaimu mratibu wa macho manispaa ya Temeke, Daniel Hebron Ringo, amesema zoezi hilo linalenga kusogeza huduma kwa wananchi ili wale ambao wamezikosa waweze kuzipata
“Kuna idadi kubwa ya wananchi wa Temeke ambao wana matatizo ya kiafya ikiwemo macho kwa hiyo kwa kulifanya zoezi hili tunawasaidia waweze kupata matibabu” amesema Ringo
Aidha Mratibu huyo ameogeza kuwa licha ya kwamba zoezi hilo ni la siku moja lakini litakuwa ni endelevu katika manispaa hiyo kadri ya watakavyokuwa wanajiandaa kwa ajili ya kumaliza tatizo la macho katika wilaya hiyo.