
Taasisi ya Mifupa (MOI) iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili imesema kuwa tatizo la kuzaliwa watoto wenye vichwa vikubwa bado ni kubwa nchini Tanzania kwani kila siku wanapokea wagonjwa wapya watoto zaidi ya 50 wenye tatizo hilo.
Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi (MOI) Bi. Flora Kimaro ameeleza hayo na kubainisha kuwa changamo kubwa inayowakabili kwa sasa ni wanawake waliojifungua watoto wenye vichwa vikubwa kutelekezwa na waume zao hali inayopelekea huduma zote za matibabu na operesheni za watoto kugharamiwa na taasisi hiyo.
Naye Mganga Mkuu wa serikali Mohamed Bakari amesema kuwa serikali inajitahidi kadri iwezavyo kugharamia matibabu ya watoto hao lakini inaiomba taasisi za binafsi na jamii kwa ujumla kushirikiana kwa pamoja katika kuwasaidia watoto hawa.