Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wasukuma domo zege waonywa wasifanye 'Chagulaga'

Jumatano , 6th Jul , 2022

Mkuu wa wilaya ya Ulanga, Ngollo Malenya, amepiga marufuku tabia ya baadhi ya vijana wa jamii ya wafugaji wa kabila la Wasukuma kuwalazimisha wanawake kwa nguvu kufanya nao mapenzi na kutaka kuwaoa bila ridhaa yao na kuwaambia mila hizo za Chagulaga zimepitwa na wakati.

Mkuu wa wilaya ya Ulanga, Ngollo Malenya

Kauli hiyo ameitoa katika Kijiji cha Igumbiro katika mwendelezo wa ziara yake ya kusikiliza kero za wananchi katika vijiji vya wilaya hiyo, jambo hilo liliibuka baada ya wanawake kutoa malalamiko yao kwake na kusema kuna baadhi ya wanaume wanalazimisha wanawake kufanya nao mapenzi ama kuwaoa bila ridhaa yao na hufanya hivyo kwa kuwavizia wakiwa wanaenda shambani au wakiwa kwenye minada.

"Suala la Chagulaga lilikuwa enzi za mabababu zetu huo ni ubakaji, kama umempenda mwanamke si uende ukazungumze nae, usione soo sema nae sasa unaenda kuvamia inaonesha mdomo wako ni mzito huna ujasiri wa kwenda kumtongoza mwanamke, domo zege," amesema DC Ngollo

Wananchi wanasema wanaume hao wakikutana na mwanamke humzunguka na kumwambia achague mtu mmoja afanye naye mapenzi, "Mwanamke akikataa anapigwa viboko kama kuna Baba yako au bwana wako akija anapigwa viboko na yeye"
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja