Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watakiwa kuinusuru Longido na ukame

Alhamisi , 12th Mei , 2016

Wananchi waishio katika wilaya ya Longido mkoani Arusha pamoja na wadau wa maendeleo wametakiwa kuinusuru na ukame kwa kupiga marufuku uchomaji mkaa na ukataji miti kwa kuhimiza utunzaji wa mazingira katika wilaya hiyo inayokabiliwa na uhaba wa maji.

Mwenyekiti wa Chama cha Wanahabari Mkoa wa Arusha Cloud Gwandu.

Mwenyekiti wa Chama cha Wanahabari Mkoa wa Arusha Cloud Gwandu, ametoa kauli hiyo wakati akizungumza katika zoezi la upandaji miti katika shule ya Sekondari Longido na Sekondari ya Tingatinga liliondeshwa na wanahabari kwa kushirikiana na wadau wa mzingira .

Gwandu amesema kuwa kutokana na ongezeko la tatizo la mabadiliko ya tabia ya nchi wanahabari wameamua kushiriki katika kurudisha uoto wa asili katika mazingira.

Alfred Mwakivike kutoka kampuni ya TGT wanaojihusisha na utunzaji wa mazingira amesema kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na ukame kwa kiasi kikubwa hivyo zoezi la upandaji miti linapaswa kuwa endelevu.

Kwa upande wao wanafunzi wa Shule ya Sekondari Longido Grace Mkambala na Omari Shafi Omari wanafunzi wa kidato cha tano wamesema kuwa tayari wameanza juhudi za kutunza vitalu vya miti ikiwa ni pamoja na miti waliyopatiwa na wanahabari ambayo itasaidia kuboresha mazingira ya shule kuwa bora na yanayofaa kwa taaluma.

Wanahabari mkoani hapa wameshiriki katika zoezi la upandaji miti ambapo kwa mwaka huu na mwaka ujao wa 2017 wanatarajia kupanda miti laki moja katika shule za sekondari za kata ikiwa ni mchango wa wanahabari katika jamii inayowazunguka.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi