Magari yaliyopata ajali na kusababisha vifo vya watu watano
Mganga Mkuu wa Hosptali ya Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya, Diodes Ngaiza, amethibitisha vifo vya watu watano na majeruhi 31 na kwamba baadhi wanaendelea kupata matibabu katika Hospitali ya Igogwe na wengine Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya.
Miongoni mwa waliofariki dunia ni pamoja na Enele Mwakalobo na Francis Mwakalobo ambao walikuwa wakielekea kwenye msiba wa ndugu yao Esther Mwakalobo.