Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watu watatu wafariki kwa ajali Mbeya

Jumanne , 3rd Dec , 2019

Watu watatu akiwemo Dereva na utingo wake, wamefariki Dunia baada ya Gari kubwa la kusafirishia mafuta, kufeli breki na kuligonga gari jingine katika kijiji cha Ibula,wilayani Rungwe, mkoani Mbeya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei.

Kamanda wa Polisi mkoani hapo, Ulrich Matei, amesema ajali hiyo iliyohusisha gari aina ya Howo, mali ya Kampuni ya Camel Oil, lililokuwa na tera lake likielekea nchini Malawi, imetokea leo Desemba 3, 2019, majira ya saa 4:00 asubuhi, katika eneo la Kanyegele maarufu kama Airport, Kata ya Kiwira, wilayani Rungwe.

Kamanda Matei amewataja waliopoteza maisha kuwa ni Frank Chota (48), ambaye ni Dereva wa gari la kusafirishia mafuta, pamoja na utingo wa gari hilo aliyefahamika kwa jina moja la Silas,wote wakazi wa Morogoro.

Mwingine ni Nelson Samson (35), ambaye ni Dereva wa gari ya kampuni ya maji ya Rungwe Spring na mkazi wa Airport jijini Mbeya.

Kwa mujibu wa kamanda Matei, chanzo cha ajali hiyo ni hitilafu kwenye mfumo wa breki wa gari lenye tanki la mafuta na kupelekea tairi moja la nyuma kushika moto na kwamba miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Rungwe – Makandana.
 

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera