Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watu watatu wafariki kwa ajali Mbeya

Jumanne , 3rd Dec , 2019

Watu watatu akiwemo Dereva na utingo wake, wamefariki Dunia baada ya Gari kubwa la kusafirishia mafuta, kufeli breki na kuligonga gari jingine katika kijiji cha Ibula,wilayani Rungwe, mkoani Mbeya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei.

Kamanda wa Polisi mkoani hapo, Ulrich Matei, amesema ajali hiyo iliyohusisha gari aina ya Howo, mali ya Kampuni ya Camel Oil, lililokuwa na tera lake likielekea nchini Malawi, imetokea leo Desemba 3, 2019, majira ya saa 4:00 asubuhi, katika eneo la Kanyegele maarufu kama Airport, Kata ya Kiwira, wilayani Rungwe.

Kamanda Matei amewataja waliopoteza maisha kuwa ni Frank Chota (48), ambaye ni Dereva wa gari la kusafirishia mafuta, pamoja na utingo wa gari hilo aliyefahamika kwa jina moja la Silas,wote wakazi wa Morogoro.

Mwingine ni Nelson Samson (35), ambaye ni Dereva wa gari ya kampuni ya maji ya Rungwe Spring na mkazi wa Airport jijini Mbeya.

Kwa mujibu wa kamanda Matei, chanzo cha ajali hiyo ni hitilafu kwenye mfumo wa breki wa gari lenye tanki la mafuta na kupelekea tairi moja la nyuma kushika moto na kwamba miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Rungwe – Makandana.
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala