
Kutolewa kwa mafunzo hayo ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa alilolitoa wakati wa ajali hiyo akiwa mkoani Kagera
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo ambayo yamewashirikisha wavuvi hao kutoka wilaya za Missenyi na Bukoba, Mkurugenzi msaidizi Idara ya maafa ofisi ya waziri mkuu, Luteni Kanali Selestine Masalamado amesema kuwa mafunzo hayo pia yatawawezesha wavuvi hao kutoa taarifa sahihi na kwa wakati, ili kupunguza madhara yanayoweza kutokea.
Novemba 06 mwaka huu ndege ya shirika la Precision Air ilidondoka katika ziwa Victoria na kusababisha vifo vya watu 19, huku wengine 26 wakiokolewa, miongoni mwao wakiwamo watu 24 waliokuwa abiria katika ndege hiyo.