Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waziri Mkuu atoa agizo Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Jumamosi , 8th Aug , 2020

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Mifugo na Uvuvi ihakikishe inaboresha utoaji wa elimu ya ufugaji bora kwa wafugaji ili kuiwezesha mifugo yao kuwa na ubora na uzito mkubwa badala ya mifugo ya aina hiyo kuonekana kwenye maonesho pekee.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu ambaye amemuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika sherehe hizo ametoa agizo hilo leo (Jumamosi, Agosti 8, 2020) katika kilele cha Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima Nane Nane Kitaifa kwenye Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu. 

Mara nyingi ng’ombe wenye uzito wa kilo mia nane, mia tisa nawakuta kwenye maonesho tu lakini hatuwaoni kwa wafugaji. Hawa anawatunza nani na kwa nini tusiwaambie wawatunze kama mnavyowatunza. Lazima tuwe na ng’ombe wanaofugwa na wafugaji wenye uzito huo, hivyo wafundisheni namna ya kuwatunza”, amesema Majaliwa.

Ameongeza kuwa, “Nimetembelea baadhi ya mabanda kwenye viwanja hivi vya Nyakabindi na nimeona bidhaa nyingi zinazotokana na mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi, huu ni ushahidi tosha wa mchango wa sekta ya kilimo katika kufikia uchumi wa kati. Tukumbuke kwamba safari yetu ya kujenga uchumi wa viwanda inaendelea".

Amesema kupitia maonesho hayo ya 28 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1993, wakulima, wafugaji, wavuvi, wanaushirika na wajasiriamali hupata fursa ya kuonesha na kujifunza matumizi ya teknolojia bora za kilimo, ufugaji na uvuvi kwa ajili ya kuongeza tija na uzalishaji wa uhakika wa chakula sambamba na kukidhi mahitaji ya viwanda na masoko ya ndani na nje ya nchi. Kauli mbiu ya sherehe hizo kwa mwaka huu ni “Kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Chagua Viongozi Bora 2020”.

HABARI ZAIDI

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera