Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waziri Ummy akiri Upungufu

Jumatatu , 21st Aug , 2017

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu amekiri kuwa nchi ya Tanzania inakabiliwa na upungufu mkubwa wa mahabusu za watoto ambapo kwa sasa kuna vituo vitano tu.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo leo wakati akikabidhiwa kisima cha maji safi kilichojengwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Dar es Salaam kwa ajili ya kuwasaidia watoto na wafanyakazi wa mahabusu ya watoto Upanga.

Waziri Ummy amesema changamoto hizo serikali imeziona na tayari mipango madhubuti imekwisha andaliwa ili kumaliza hali  ya kuwachanganya watoto na watu wazima ambayo siyo sahihi.

Katika hatua nyingine Mhe. Ummy amesema kisima hicho alichokabidhiwa leo kitazalisha lita 5,000 kwa siku na kuokoa gharama za kila mwezi kwa serikali ambazo zilikua zinatumika kulipia huduma hiyo ambapo fedha hizo zitabadilishwa matumizi kwa kuwafungulia bima za afya.

Kwa upande wa Kadinali Pengo kwa upande wake amesema katika misaada yao ambayo wamekuwa wakiitoa kwa jamii wanaepuka kuitoa kwa ubaguzi wa aina yoyote.

"Tunaweza kufanya hayo japo yanaweza kuonekana ni madogo lakini sisi tunasukumwa na upendo, hivyo tukifika mahali hatuulizi wewe ni dini gani au dhehebu gani tunapenda amani na upendo udumu kwenye jamii,"alisema

Chanzo cha kuchimbwa kisima hicho ni kutokana na ziara waliyoifanya watoto wa Shirika la Utoto Kurasini kituoni hapo na kubaini changamoto inayowakabili watoto wenzao, hivyo wakaguswa na kuomba ushirikiano na vikundi vingine vilivyowezesha kujengwa kwa gharama ya Sh 11,780,000.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi