Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wengine wawili wajiuzulu CHADEMA

Jumatano , 21st Feb , 2018

Madiwani wawili wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutoka kata za Terati na Daraja mbili katika Jiji la Arusha wamejiuzulu nyadhifa zao na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Madiwani hao ni pamoja na Prosper Msofe (Daraja mbili na Obeid Meng'oriki (Terati) ambao kwa pamoja wameamua kujiunga na CCM ili kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais Dkt. John Magufuli.

Msofe ambaye aliwahi kuwa Naibu Meya wa Jiji la Arusha (CHADEMA) amesema Mbunge wa jimbo hilo Godbless Lema hataki mtu mwenye uwezo mkubwa katika chama na mara zote humpiga vita.

Naye Diwani wa Kata ya Terati  Meng'oriki amesema CHADEMA ni chama cha kihalifu, kifitini na kilichojaa chuki, ubaguzi, urasimu mkubwa huku akidai endapo ikitokea makada wa chama hicho wakimsifia Rais Magufuli kwa kazi nzuri anayofanya huwa wanakemewa vibaya.

Kwa upande mwingine, Katibu wa CCM wilaya ya Arusha Musa Matoroka amesema madiwani hao wameamua kujiunga na CCM ili kumuunga rais mkono na kuahidi kushirikiana na wananchi hao na kuwataka vigogo wa CHADEMA kuacha kupiga propaganda na siasa za uchwara kuwa kila diwani anayehama chama hicho amenunuliwa.

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya