Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wizara nne zatakiwa kutoa suluhu migogoro ya ardhi

Alhamisi , 3rd Mar , 2016

Waziri Mkuu Kasim Majaliwa amewataka mawaziri wa wizara nne kukaa na kutafuta suluhisho la pamoja na la kudumu la migogoro ya ardhi na mipaka ili kuepusha madhara yanayotokana na migogoro hiyo.

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa

Waziri Mkuu Majaliwa ametoa agizo hilo akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Simiyu ambapo pia amewahakikishia wakazi wa wilaya ya Busega kuwa serikali itamaliza migogoro yote ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji wilayani humo.

Kauli hiyo imekuja baada ya Mbunge wa Busega Rafaeli Chageni kuwasilisha kilio cha wananchi kukosa sehemu ya kulima kutokana na wawekezaji kuchukua maeneo makubwa kinyume na taratibu na wengine kughushi nyaraka za umiliki wa ardhi.

Waziri Majaliwa amewataka Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe Jumanne Maghembe, Waziri wa TAMISEMI, Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Ardhi Mhe. William Lukuvi, na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mwigulu Nchemba kutatua mgogoro huo.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watumishi na watendaji wote wa serikali wahamie yalipo makao makuu ya wilaya ya Busega kuanzia sasa ili kuleta kasi ya utendaji kazi kwenye wilaya hiyo ambayo ni mpya wafanye mapitio ya maeneo yote yenye migogoro ya ardhi.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo wakati akizungumza na wananchi waliofika kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi kwenye jengo la utawala la halmashauri ya wilaya ya Busega mkoani Simiyu.

Waziri Mkuu ambaye ameanza ziara ya siku sita ya mkoa huo atakagua shughuli za maendeleo na kusalimia na wananchi katika wilaya zote za mkoa huo.

Waziri Mkuu alisema kitendo cha watumishi kuhamia yalipo makao makuu ya wilaya kitasaidia kuongeza kasi ya kuleta maendeleo kwani watakuwa wanaziona changamoto zilizopo mahali wanapoishi.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea