Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Zaidi ya watu laki tatu waandikishwa na BVR,Njombe

Alhamisi , 23rd Apr , 2015

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)imesema kuwa emeandikisha watu zaidi 300,000 na kuwa imekamilisha katika mkoa huo na itaanza mwezi mei katika mikoa ya Dodoma, Mbeya, Rukwa na Katavi na mwezi huu ikianza katika mikoa ya Iringa, Ruvuma,Lindi na Mtwara

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Damian Lubuva akifafanua jambo.

Akizungumza kwa njia simu mwenyekiti wa tume ya taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Damian Lubuva amesema kuwa zoezi BVR kwa mkoa wa Njombe limekamilika na kuwaandikisha wananchi zaidi ya 380,000 katika mkoa huo.

Jaji Lububa amesema kuwa baada ya kukamilika mkoani Njombe zoezi hilo linaelekea katika mikoa ya Iringa, Ruvuma, Lindi na Mtwara ambapo linatarajiwa kuanza Aprili 24, mwaka huu.

Amesema kuwa mbali ya mikoa hiyo ambayo imeanza mwezi huu pia ilitaanza ndani ya mwezi Mei ambayo ni pamoja na mikoa ya Dodoma, Mbeya, Rukwa na Katavi.

Amesema kuwa katika mkoa wa Njombe limefanikiwa vizuri kwa kuandikisha watu zaidi ya 380,000, na kuwa haoni sababu ya uchaguzi mkuu kuahirishwa Oktoba, kwa sababu wana vifaa 1,600 kwa sasa kutoka 250 vilivyokuwepo awali, na kwamba wiki ijayo wanatarajia kupata 1,600, na hivyo kufikia 3,200 ambavyo watavitumia katika mikoa ya Iringa, Ruvuma, Lindi na Mtwara inayotarajia kuanza zoezi la uandikishaji.

Lubuva amesema wanatarajia hadi kufikia mwezi Mei vifaa vyote vitakuwa vimekuja na hivyo kufikia idadi ya mashine 8,000 ambazo zitafanya zoezi hilo kufanyika katika mikoa yote iliyobaki nchini.

“Mkoa wa Njombe zoezi limeenda vizuri na tumefanikiwa kuandikisha watu laki tatu na themanini hivyo sioni sababu ya uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu kuahirishwa,” alisema Lubuva.

Aidha Lubuva aliongeza kuwa pamoja na changamoto zilizojitokeza katika mkoa wa Njombe, Lubuva alisema zoezi hilo lililomalizika Jumamosi iliyopita lakini limefanyika kwa mafanikio.

Kuhusu zoezi hilo kurudiwa katika kata za Mjimwema amesema hakuna mwananchi aliyejitokeza akaachwa na yeye kama Mwenyekiti anasema hakuna yeyote aliyejitokeza.

Aidha amesema kuwa hakuna sababu ya uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani kuahirishwa Oktoba mwaka huu, kwa kuwa zoezi la uandikishaji wananchi kupitia mfumo mpya wa kielektroniki (BVR) litakuwa limemalizika.

Kauli hiyo ameitoa wakati atoa tathmini ya zoezi la uandikishaji katika mkoa wa Njombe na mwelekeo wa tume hiyo kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi