Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hamphrey Polepole.
Polepole ameyabainisha hayo leo Mei 22, 2020, Jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na waandishi wa Habari katika ofisi za chama hicho zilizopo Lumumba, na kusema kuwa isingekuwa maono ya Rais Magufuli ya kuzuia kila mtu kutoa taarifa za ugonjwa wa Corona, basi hali isingekuwa nzuri.
"Chama kilikaa muda kikatafakari kikasema, hivi si tumekua maisha yetu yote mtu akipiga chafya tunamuambia afya!, leo ukipiga chafya imekuwa ni hukumu unaweza ukachukuliwa hatua, tukaseme tujiongeze tuchukue hatua, na ndiyo maana hata hili jambo la kufungia watu ndani kama mifugo, Mataifa makubwa wananchi wanaandamana" amesema Polepole.