Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Namthamini yaipiga jeki Kisarawe kuinua elimu

Jumapili , 11th Oct , 2020

Wilaya ya Kisarawe imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kuinua elimu ya mtoto wa kike zikiwemo za kutenga fedha kwa ajili ya kuwanunulia taulo za kike pamoja na kujenga shule ya sekondari ya bweni ya wanafunzi wakike.

Timu ya East Africa Tv na Radio ikimkabidhi Taulo za kike Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani yaliyofanyika kwenye shule ya Sekondari Minaki.

Mwegelo amesema  halmashauri imekuwa ikitenga fedha za kununulia taulo za kike ambapo mwaka jana ilitenga sh. milioni 4 na mwaka huu sh. milioni 3, jitihada ambazo pia zimekuwa zikiungwa mkono na EATV kupitia kampeni yake ya Namthamini.

Awali akifungua maadhimisho hayo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Kisarawe, Mussa Gama, amesema kuwa wilaya ya Kisarawe bado inakabiliwa na tatizo la mimba za utotoni ambapo hatua mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa kudhibiti hali hiyo.

Kampeni ya Namthamini imefanikiwa kupatikana kwa taulo za kike zinazokidhi mahitaji ya wanafunzi wa kike 300 kwa mwaka mzima, pamoja na vifaa vingine vya shule.

Awali maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Kisarawe kwa kushirikiana na EATV kupitia kampeni ya Namthamini yalianzia ofisi ya Mkuu wa Wilaya Kisarawe hadi shule ya Sekondari Minaki.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja