Alhamisi , 7th Jan , 2021

Ni 'Headlines' za msanii wa BongoFleva Barakah The Prince ambaye amenyoosha maelezo kwa kusema asilimia 85 ya muziki unaoimbwa sasa ni kelele, fujo na wasanii wanaimba bora wimbo utrend tu bila kuangalia topic.

Msanii Barakah The Prince

Akieleza hilo kupitia post yake aliyoweka kwenye mtandao wa Instagram Barakah The Prince anasema 

"Leo nimejaribu kupitia baadhi ya nyimbo mpya zimetoka hivi karibuni, nimegundua katika 85% ya miziki hiyo ni kelele nyingi, miziki iliyokosa topic yaani fujo fujo tu bora li-trend, bora liendee na bora walevi waka-bang, twapaswa kujitafakari wanamuziki wa kizazi hichi cha nyoka

Barakah The Prince ni mmoja wa wasanii ambao wanauwezo wa kuandika na kuimba nyimbo zenye hisia kali za mapenzi.
 

Bonyeza hapa kutazama Interview ya Hamis Bss akimlilia Harmonize