
msanii wa miondoko ya Hip Hop nchini Adili aka Hisabati
Adili ambaye ni mmiliki wa studio ya chapakazi mkoani Mbeya ameelezea kuwa studio yake hiyo imejipanga kuanza matayarisho makubwa ya kuandaa show itakayokuwa mahususi kwa ajili ya kuinua aina ya muziki huo.
Aidha rapa huyo wa studio hiyo ya chapakazi ambaye licha ya kuwa promota na mtayarishaji mkuu wa studio hiyo amesema kuwa huu ni mwaka wa kuanza kuirudisha hip hop katika chati.
