Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Alikiba aahidi kufanya kazi na 'madansa' #Dance100

Jumapili , 25th Sep , 2016

Msanii wa Bongo Fleva Alikiba ameahidi kuchukua baadhi ya vijana walioshiriki hatua ya fainali ya shindano la Dance100% 2016.

Msanii Ali Kiba ambaye ameshiriki kama jaji mgeni Dance100%

Akizungumza na EATV Alikiba amesema uwezo uliooneshwa na makundi yaliyoshiriki umemfanya aone kuna sababu ya msingi ya kukuza vipaji vyao kwa kuchukua baadhi ya waliofanya vizuri na kuwajumuisha kwenye kazi zake.

“Nashukuru kwa kuwa Jaji mgeni katika hatua hii ya fainali, jambo ambalo limenifanya nione namna ambavyo kuna vipaji vingi sana katika jamii yetu na kuna baadhi ya vijana nitawachukua kufanya nao kazi katika shughuli zangu za muziki” Amesema Alikiba

Aidha ameupongeza uongozi wa EATV kwa namna ambavyo umebuni namna ya kukuza vipaji vya wasanii kwa kuanzisha shindano la Dance100% maana kuna vipaji vingi sana ambavyo vinavumbuliwa na wengi wanaweza kupata ajira na kutambulika kupitia Dance100%.

Pamoja na hayo Alikiba amewataka washiriki ambao wameshindwa kushika namba moja au mbili wasikate tamaa kwani katika maisha kujituma ni njia ya kupata mafanikio.

Shindano la Dance100% 2016 limefikia hitimisho leo kwa makundi 6 kupambana ambapo kundi la Team Makorokocho limeibuka na ushindi na kujinyakulia kitita cha milioni 7.

Matukio yote ya Dance100% yataoneshwa kupitia kituo cha EATV siku ya Jumapili kuanzia saa moja jioni ambapo shindano limedhaminiwa na Vodacom kwa kushirikiana na Coca- Cola.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi