Picha ya msaniI Snura Mushi
Snura Mushi amesema hayo kupitia show ya Planet Bongo ya East Africa Radio, ambayo inaruka kila siku za Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia 7:00 mchana mpaka 10:00 jioni.
"Mambo hayo ya Alkasusu, Urojo, juisi ya tende na mihogo mibichi vyote vipo mwilini mwangu akinigusa tu anavipata, kila siku kwetu ni Valentine Day penzi letu lipo juu kama dirisha la chooni, halafu kuhusu umri nimemzidi miaka kidogo sio mingi kihivyo kama watu wanavyofikiria" amesema Snura Mushi.
Pia wapenzi hao wamekiri kuwa waliachana kipindi cha nyuma na wamesema sababu ya kuachana kwao ni mambo ya nje kuwa mengi kuliko mapenzi yao.
"Tuliachana kweli kuna vitu tulipishana kidogo ila kuachana sio kufa,nafikiri mambo yanakuwa mengi kwetu sisi, watu wanaongea vitu vingi sana, hakuna kitu chochote kibaya alichonifanyia hakunisaliti wala sijakuta message yoyote mbaya, maana hayo ndiyo makosa makubwa ya watu kuachana" Snura Mushi na Minu Calypto.