
Dhamana hiyo imetolewa leo, Novemba 27 ambapo Amber Rutty amedhaminiwa na ndugu yake, huku mpenzi wake akidhaminiwa na Mchungaji Daudi Mashimo wa Kanisa la Emmaus Bible Church, Mbezi Luis DSM.
Hapo jana Hakimu Mkazi Mkuu, Augustine, Rwezire alisema dhamana ya wawili hao bado iko wazi, ambapo ilikuwa ikihitaji wadhamini ambao kila mtu atasaini bondi ya Shilingi Milioni 15, wawe na vitambulisho vya taifa pamoja na kuwasilisha hati za kusafiria, pia wasitoke nje ya Dar es Salaam bila ruksa.
Ikumbukwe kwamba Mchungaji Daudi Mashimo ndiye aliyetangaza kufanya maombi maalum kwa Wema Sepetu, na kumtaka muigizaji huyo kuokoka ili kuondokana na mikosi inayomkabili katika maisha yake.