Jumamosi , 20th Apr , 2019

Bodi ya Filamu nchini imetoa tamko lake juu ya kauli iliyotolewa na Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku ‘Msukuma’ kuwa bongo movies imekufa na wasanii wanategemea michango ya misiba, na kusema kwamba kauli hiyo inadhalilisha bodi hiyo na wasanii.

Taarifa ya tamko hilo imetolewa kwneye barua maalum iliyotolewa na Bodi ya Filamu nchini, na kusema kwamba ni kuidhalilisha taaluma na kutaka kuwaaminisha watanzania kuwa wasanii ni wapigaji wa pesa za rambirambi, jambo ambalo si sahihi.

Barua iliyoandikwa na Bodi ya Filamu

 

Barua iliyotolewa na bodi ya filamu

Hata hivyo wasanii wa filamu za bongo nchini walisema wanajipanga kwenda jijini Dodoma kwa lengo la kumpongeza Musukuma, kutokana na kupigania haki za wasanii wa tasnia hiyo kwa kusema ukweli halisi uliopo kwenye maisha yao.