Jumatano , 23rd Jun , 2021

Swizz Beatz, Busta Rhymes na wasanii wengine waliowahi kufanya kazi na The late Rapper DMX watapata nafasi ya kufanya show ya kutoa heshima kwa mkongwe huyo kwenye  tuzo za BET zinazotarajiwa kufanyika siku ya Jumapili, Juni 27, 2021.

Picha ya msanii DMX

Rapper DMX anakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwenye sanaa na ushawishi aliokuwa nao duniani kote kupitia muziki huku akishikilia rekodi ya kuwa msanii pekee katika historia kuwa na album tano mfululizo kushina nafasi ya 1 kwenye chart za Billboard 200 na Top R&B/Hip-Hop huku akiwa ameuza zaidi ya kopi milioni 74, ana album/single 14 zilizouza zaidi ya kopi milioni 1 nje na ndani ya Marekani.

DMX alifariki aprili 9, 2021 akiwa na umri wa miaka 50.