Jumamosi , 2nd Mei , 2015

Prince Dully Sykes msanii anayeshikilia game ya Bongo Flava kwa miaka mingi sasa, amesema kuwa rekodi yake mpya ya shuka ni maalum zaidi kwa mashabiki wake kutoka Mombasa, wakifuatiwa na wale wa maeneo mengine ndani na nje ya Afrika Mashariki.

Prince Dully Sykes

Dully Sykes amesema kuwa, amekuwa na Love sana na mashabiki wake kutoka Mombasa zaidi ya sehemu nyingine kutokana na mapenzi yao makubwa kwa kazi zake na yeye binafsi.

Staa huyo ambaye hajawahi kukosea katika mlolongo wa rekodi zake mpaka leo, amejitaja mwenyewe kama Rais wa Mombasa, huku eNewz ikiendelea kufanya uchunguzi wa karibu juu ya kile hasa ambacho mashabiki kutoka eneo hilo wamempatia na kumfanya awakubali zaidi ya mashabiki wake wengine.