Gari ambayo amepata nayo ajali Esha Buheti
Kupitia katika ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, Esha Buheti amepost picha ya gari ambayo amepata nayo ajali katika daraja la Wami mkoani Tanga ambapo ameandika "Ahsanteni kwa message zenu na simu nyingi sana nimezipata ila kwa sasa kicha kinauma sana, ni kweli tumepata ajali ila tumetoka salama alhamdulillah"
Aidha muda mfupi uliopita kupitia mtandao huohuo wa Instagram amepost video fupi ya gari alilopata nalo ajali likiwa limebebwa na kuandika,
"Tunaanza safari ya kurudi Dar, nasikitika sana kwa habari zinazoendelea kuhusu ajali hii, nimekaa kimya sana ila muda wa kuongea umefika, nimechoka kwenye maisha yangu sijawahi kumtapeli wala kumuibia mtu" ameandika
Mimi sio mtu wa maneno maneno ndiyo maana kwenye maisha yangu nipo kivyangu na kazi zangu, nimekaa kimya sana ila imezidi mara naishi maisha ya uongo, mara nimemkuwadia mtu mwanaume na nipo tayari kuongea na waandishi wa habari muda wowote" ameongeza