Kwenye ukurasa wake mnamo februari 9, Godzila aliandika ujumbe kuwa hata kama akifa, jina lake litaendelea kubaki kwa watu, jambo ambalo limetafsiriwa kama alikuwa anakaribia kufikwa na umauti.
Even if I die today my name gona be here ....jokes on you https://t.co/fxBjUpBgul
— GOLDEN JACOB (@King_Zillah) February 9, 2019
Hata hivyo Godzilla aliendelea kutumia ukurasa huo mpaka jana saa 9 alasiri, ambapo alitweet ujumbe wake wa mwisho, ambao ulisomeka hivi.
N no info ssheesh
— GOLDEN JACOB (@King_Zillah) February 12, 2019
Kutokana na kifo cha Godzilla Rais mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete, ametoa ujumbe uliolezea kusikitishwa kwake na msiba huo, huku akisema kwamba Godzilla alikuwa na ndoto nyingi ambazo zimezimika ghafla
Nimestushwa na taarifa za kifo cha msanii wa kizazi kipya GodZila. Alikuwa kijana mdogo mwenye ndoto kubwa na ameondoka wakati ambapo bado mchango wake ulihitajika. Nawapa pole familia ya Marehemu na wasanii wote kwa msiba huu. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema. pic.twitter.com/eySOXLdg5u
— Jakaya Kikwete (@jmkikwete) February 13, 2019