Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

H Baba aanika ukweli kuhusu ndoa yake

Ijumaa , 5th Apr , 2019

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Hamisi Ramadhani maarufu kama H Baba, amezungumzia suala la kutalikiana na mkewe Flora Mvungi, na kusema kwamba hajamtaliki mkewe kama inavyodaiwa.

Akizungumza na www.eatv.tv, H Baba amesema kwamba kitu anachojua ni kwamba Flora bado ni mkewe kwani yeye ndiye aliyeoa, hivyo kama ni talaka yeye ndiye mwenye kuitoa lakini kamwe hajafanya hivyo.

H Baba ameendelea kusema kwamba kauli ya Flora kuwa ndoa ya wawili hao imekufa sio kweli, na kama Flora ndiye aliyeoa basi atoe talaka ili kuvunja ndoa hiyo.

H Baba akifunguka zaidi 

 

“Maisha yangu ya muziki hayaingiliani na familia yangu na watoto, sikumuoa instagram, kwa sababu unapozungumza ili watu wakusikie, ili u-trend sio kitu cha busara kwa sababu unaongea uongo, mimi ninachojiua ni mtu ambaye sijampa talaka, na mtu ambaye hatuna ugomvi, mimi niko busy na baishara zangu".

“Kwa mfano mimi ningekuwa nimefungwa miaka mitano angeniacha!?. Na yeye ni mke wangu, mimi nimemuoa kwa dini na sheria za Kiislam, kwa hiyo kama ataomba talaka atanitafutia mke, atanitolea mahali atanipa huyo mke nitatoa talaka, mimi ninachojua yeye ni mke wangu. Wanaosema nan'gang'ania, mwanaume anang'ang'ania ndoa!?. Mimi naangalia watoto wangu, lakini hajaniomba na tupo vizuri, yule ni mke na atabakia kuwa mke”, amesema H Baba.

Hivi karibuni kumekuwa na mvutano kati ya wawili hao kudai kuwa wameachana. Taarifa ambayo imetolewa na mwenyewe mke wa H Baba, Flora Mvungi huku H Baba akiendelea kukanusha kuwa hajamtaliki mkewe na bado wako vizuri.

H Baba akiwa na mkewe na wasimamizi wao siku ya harusi

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani