Jumatatu , 11th Dec , 2017

Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye hivi karibuni amemaliza tofauti zake na msanii mwenzake Lady Jaydee baada ya kutokuwa na maelewano mazuri kwa muda mrefu, amesema hakuna mtu aliyemuomba msamaha mwenzake kati yao ili kuyamaliza.

Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Mwana FA amesema ugomvi wake na Jaydee hakuna mtu aliyewakalisha kujaribu kuwapatanisha au wenyewe kuombana msamaha, bali waliumaliza kwa yeye kumpigia simu, na kuzungumza kama ambavyo wengine wanazungumza, 

"Hakuna aliyemuomba msamaha mwenzake, mi ndio nilianza, nilimtumia meseji oya vipi, akajibu fresh, nikamwambia FA hapa usiku nilikutafuta, akajibu mimi siku hizi nimezeeka nalala mapema, ndo hivyo tukayamaliza hivyo", amesema Mwana FA.

Mwana FA ambaye kwa sasa ameachia kazi mpya aliyomshirikisha Maua Sama, amesema licha ya kumaliza tofauti zao na Jaydee, watu wasitarajie sana kazi ya pamoja kwani kibinadamu itaonekana wamemaliza tofauti hizo kwa ajili ya kazi.

Itazame kazi mpya ya Mwana FA ft Maua Sama 'Hata sielewi' hapa