Ijumaa , 7th Mei , 2021

Kwenye game ya BongoFleva zimeimbwa nyimbo nyingi sana za simulizi yaani 'story telling' na zinafanya vizuri mpaka leo, sasa hizi hapa ni baadhi ya 'hit songs' ambazo zina simulizi ila zimeacha maswali baada ya wimbo baada verse za wimbo kumalizika.

Picha ya msanii Mwana Fa kushoto, kulia ni Ferooz

1. Alikufa kwa ngoma

Mhe Mbunge wa Muheza Mwana FA hakuamini kama jamaa anaweza kufa kwa Ukimwi na alijiuliza swali ambalo mashabiki wake mpaka leo wanajiuliza alipataje Ukimwi (ngoma) licha ya kuwa na maisha ya kitakatifu na mtu wa dini sana, Mwana Fa alitumia mistari mingi kuthibitisha kwamba jamaa alikuwa 'innocent' kiasi gani.

Mwisho Mwana Fa anasisitiza jamaa alikufa kwa ngoma, mpaka leo hakuna mtu anayejua alipataje Ukimwi alizaliwa nao aliambukizwa, ngoma hiyo ilitoka mwanzoni mwa miaka ya 2000 na alimshirikisha Lady Jaydee.

2. Rita

Video ya ngoma hii ya Rita ina 'views' Milioni 2 mjini YouTube, ilikuwa safari ya Arusha kuja Dar, Marlaw ametuelezea kwamba Rita alifariki kwenye gari lakini bahati mbaya ni kwamba sio Marlaw,Daktari Dereva, Konda wa gari Abiria au jirani wa Rita ambaye anajua nini chanzo cha kifo cha Rita. Hii ni hit song nyingine ambayo imeacha maswali kwa watu kwamba nini kilimuua Rita.

3. Story

Kwenye ngoma ya story ambayo Soggy Doggy aliwapa shavu Mandojo na Domokaya, Soggy alituacha na swali kwamba baada ya ajali yule dada Recho alipatwa na nini, kwa sasabbu mwanzo wa ngoma Soggy anasema alikuwa akiongea vizuri lakini baada ya ajali kila akipiga namba inapokea ila haiongei.

Swali ni kwamba dada alikufa, alipona au alipata shida ambayo ilimfanya ashindwe kuongea au kitu gani kilimpata.

4. Boss 

Moja kati ya ngoma ambayo ina dakika nyingi kwenye BongoFleva basi ni hii ya 'Boss' ambayo ina dakika 7 'verse jamvi' Ferooz ambayo amemshirikisha Juma Nature na Solo Thang, Ferooz ametupa stori ambayo mke wake alitoka na boss kimapenzi hadi kumpa ujauzito.

Ferooz anasema akimuuliza mkewe suala hilo anakataa na anaogopa kumuambia boss wake ukweli kwa sababu ya kuhofia kukosa kazi akabaki kujiuliza aangamie, avumilie au akose ajira, kwa upande wa Juma Nature na Solo Thang walikuwa wanamshauri kuhusu tukio hilo.

Swali ambalo bado lipo mpaka leo ni kwamba Ferooz alifanya nini, aliachana na mkewe, aliacha kazi au aligombana na boss wake.