Jumatano , 17th Jan , 2024

Bila uoga King Of Philadelphia ‘Philly’ Meek Mill amemwambia Rais wa 46 wa Marekani Joe Biden mwenye miaka 81 kuwa ni mzee sana kuongoza Taif hilo.

Picha ya Rais wa Marekani Joe Biden na Meek Mill

Meek Mill ametuma ujumbe huo kupitia page yake ya mtandao wa X akiandika

“Joe Biden ni mzee sana kuwa rais wetu kwa heshima, Kitu gani kinaendelea katika mfumo wa Marekani ambao unasukuma haya yote kwamba ni sawa kuamini tunachokiona”.

Meek Mill amefunguka hilo baada ya Joe Biden kuwaambia ripota kuwa tayari ameshawatumia ujumbe Iran kwa kile kinachoendelea lakini Iran bado wameishambulia Ubalozi mdogo wa Marekani na Uwanja wa Ndege Kaskazini mwa Iraq.