Muigizaji Shamsa Ford
Shamsa Ford amesema hivyo kupitia EATV & EA Radio Digital, baada ya kuulizwa ni jambo gani ambalo hawezi kuamini endapo ataambiwa na mtu yeyote.
"Jambo ambalo siwezi kuliamini kabisa ni pale ukiniambia hali ngumu nakukatalia, kwa sababu ninachokiona sasa hivi hali sio ngumu ukifanya kazi pesa zipo, ila kwa wale wanaopenda njia fupi, wanaojipatia pesa kwa njia ambayo siyo sahihi au rahisi ndiyo wanaona hali ni ngumu" amesema.
"Lakini mbona nikikaa dukani na kupambana naona pesa zinakuwepo, ukiniambia hali ni ngumu naweza kukupiga hata vibao ni uongo tu, labda wanasema hali ngumu kwa sababu wanashinda nyumbani hawataki kwenda kutafuta ila kama unatoka kutafuta hali siyo ngumu kabisa" ameongeza.