
Mwana FA
MwanaFA amesema kuwa, ingawa mawazo ya watu wengi yamejengeka katika kwenda shule ili kupata cheti na kuajiriwa, kuna haja ya kubadilisha mtazamo hususan kwa wasanii kwenda shule kwa lengo la kupanua mawazo, ili kuleta maana zaidi katika kazi zao na namna ya kushughulikia mambo yao na kusimamia kazi zao.
Mana FA, aka. Tiger Woods wa Rap Bongo, aka The ChoirMaster, amesisitiza kuwa, wasanii wakisoma, kutatokea mabadiliko makubwa yenye manufaa kwa mashabiki kupitia kazi watakazotengeneza.