Alhamisi , 2nd Apr , 2020

Mrembo na Video Vixen Nicole Joyberry, amesema anapenda mwanaume yeyote mwenye rangi nyeusi kwa sababu anaona atamfaa kwenye matumizi yake.

Picha ya mrembo na video vixen Nicole Joyberry

Akipiga stori kupitia show ya eNewz ya East Africa TV, inayoruka kila siku ya Jumatatu hadi Ijumaa, kuanzia 12:00 jioni hadi 12:30 jioni, ambapo ameeleza kuwa mwanaume mweusi atamfaa kuanzia urafiki, undugu na wanavutia.

"Mimi napenda mwanaume yeyote mwenye rangi nyeusi anayevutia, mweusi yeyote atanifaa kwa matumizi ya ki Mungu, kiurafiki au hata kindugu na sio kuwazia kwenye vitanda tu" amesema Nicole Joyberry.

Aidha mrembo huyo yupo katika video ya wimbo wa "bedroom" ya Harmonize amezungumzia juu ya kufanya kazi na msanii huyo, ambapo kwenye video wameonekana kujiachia sana.
 
"Najuana na Harmonize kabla ya hii video, wala hatujavutiana na haijaniletea madhara makubwa japo nilikuwa na mwanaume wangu namuelewa baada ya kuona akanipiga chini, sasa hivi sina tena mpenzi nipo single".