Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mzee wa Upako aichambua Muziki ya Darassa

Jumanne , 21st Feb , 2017

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo 'Mzee wa Upako' ameichambua ngoma wa msanii wa bongo fleva, Darassa inayokwenda kwa jina la Muziki, na kusema kuwa msanii huyo ameimba vitu vya maana sana kwenye ngoma hiyo.

Mchungaji Lusekelo ambaye amewahi kunukuliwa akitumia maneno ya wimbo huo na nyingine kadhaa za bongo fleva katika mahubiri yake, alikumbana na maswali katika kipindi cha KIKAANGONI cha EATV, ambapo watu walitaka kujua ni kwanini anatumia muziki wa kidunia katika mahubiri yake, badala ya nyimbo za injili.

Akijibu maswali hayo, Mzee wa Upako amesema yeye kama mwanajamii, anaishi duniani pamoja na wana jamii wengine, hivyo ni lazima ajue matatizo yanayowazunguka watu wake ili aweze kuwasaidia na ndiyo maana anajaribu kufuatilia mambo yanayopendwa na watanzanie ikiwemo muziki wa kidunia.

"Muziki ni muziki, hakuna wa kanisani wala duaniani, cha msingi ni ujumbe tu... Sasa ukisema wacha maneno weka muziki, kuna shida shida gani? Ule muziki mi naupenda sana, anasema hakuna jambo gumu kama kumfundisha chizi, na pia ni ujinga sana kusubiri embe chini ya mnazi. Mimi nina nyimbo nyingi hata za kihindi nasikilizaga sana" Alisema

Mbali na ngoma ya Darassa, pia ametoa ufafanuzi wa maamuzi yake ya kuimba wimbo wa Navy Kenzo unaokwenda kwa jina la 'Kamatia Chini', huku akishauri wasanii wa bongo fleva kuimba nyimbo zenye mafunzo badala ya nyimbo za mapenzi pekee.

"Wasiimbe nyimbo za mapenzi tu, walipe pia sadaka kwa taifa... wakati mwingine waimbe na nyimbo ambazo zinaasa maadili"

Kuhusu Diamond na Alikiba, Mzee wa Upako amesita kusema ni yupi anayemkubali zaidi, na kusema kuwa wote ni wa Mungu, na vipaji vyao vimetoka kwa Mungu.

Huyu hapa Mzee wa Upako, akiimba ngoma ya Muziki, Kamatia chini, pamoja na nyimbo kadhaa za zamani

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani