Akitoa maono hayo ya utabiri, ambayo anadai ameoteshwa na Mungu wake, Mashimo ameanza kumshukuru na kumtia moyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli kwa utendaji wake mzuri wa kazi uliotukuka na kuwatetea watanzania walio wanyonge.
“Mungu amenionyesha majimbo ya Ubunge ambayo yatapotea mwaka 2020, Jimbo la kwanza ni Arusha Mjini, ambalo linaongozwa na Godbless Lema, Pili ni Mh. Joseph Mbilinyi mbunge wa Mbeya Mjini, Tatu ni mwenyekiti wa chama cha Chadema Mh. Freeman Mbowe ambaye anaongoza Jimbo la Hai , mwisho ni Zitto Kabwe mbunge wa Kigoma Mjini” amesema Mashimo.
Nabii Mashimo ameongeza kuwa kama wabunge hao watataka kushinda nafasi zao za uwakilishi wa wananchi katika Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, amesema suluhisho pekee ni wao kutubu na kuokoka.