Alhamisi , 23rd Apr , 2026

Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group Joseph Kusaga ameweka wazi mahaba yake mazito kwa kazi ya mkongwe wa Hip Hop nchini Chidi Benz mpaka kufikia hatua ya kumuomba msanii huyo amuimbie moja wa Wimbo wake akiwa Kaburini kabla ya kupumzishwa.

Joseph Kusaga akizungumza ndani ya kipindi cha PlanetBongo amefunguka kwa kusema wimbo wa "Dar es Salaam Stand Up" ni zaidi ya burudani kwake ni wimbo unaobeba hamasa kubwa katika maisha yake ya kila siku na kumuomba Chid Benz iwapo atatangulia mbele ya haki kabla yake basi kabla ya kuingia Kaburini amuimbie wimbo huo.