Jumanne , 12th Dec , 2017

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Tunda Man ambaye mwaka huu aliuaga ukapera, amesema alipofanya uamuzi wa kuoa hakuwa na uhakika na uamuzi huo, kwani alihisi kama mwanamke wake hana mapenzi ya dhati na yeye.

Tunda Man ameyasema hayo alipokuwa akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kwamba kutokana na umaarufu alionao, alikuwa na mashaka iwapo mpenzi wake huyo alikuwa anampenda au alikuwa anafuata umaarufu.

“Kwenye kuoa nilikuwa mguu ndani mguu nje nikijuliza huyu anampenda nani, Tundaman au Khalid, baada ya kukaa naye ndio nimegundua anampenda Khalid na sio Tunda Man, nilikuwa sina uhakika kabisa na ile ndoa”, amesema Tunda Man.

Hivi sasa msanii huyo ameachia kazi mpya inayoitwa 'toto', ambaye mwenyewe amedai ni moja ya kazi bora ambazo amewahi kuzifanya tangu aanze muziki.